Last Updated on October 13, 2023 by Dr Mniko
KASWENDE NI NINI?
Kaswende ni ugonjwa wa ngono unaosababishwa na bakteria anyeitwa Treponema pallidum. Kama ugonjwa wa kaswende hautatibiwa unaweza kusababisha matatizo makubwa. Habari njema ni kwamba, kaswende inaweza kutibiwa vyema na penicillin au aina nyingine za antibiotiki.
Ni zipi hatua na dalili za kaswende?
Kaswende ina hatua nne inazopitia, kutegemea ni kwa muda mtu amaekuwa na huu ugonjwa. Kila hatua inaweza kuwa na dalili tofauti.
Hatua ya mwanzo ya ugonjwa – kama umeambukizwa hivi karibuni, unaweza kuwa na kidonda kigumu kwenye mlango wa uke au uume. Kidonda hiki kinaitwa chacre. Kwa kawaida kuna kidonda kimoja kisicho na maumivu, lakini kunaweza kuwepo na vingi.
Kama usipotibu hatua ya mwanzo ya ugonjwa wa kaswende, inaingia katika hatua ya pili. Unaweza kuwa na dalili kama za mafua na upele mwili mzima. Unaweza kuwa na vijinyama vinavyoota kwenye Ngozi vinavyoitwa condyloma latuma. Mara nyingi vijinyama hivi huota karibu na uke au uume au karibu na mkundu. Unaweza pia kuwa na matatizo kwenye figo, ini, na viungo vingine
Hatua inayofuata ni hatua ya tatu ya ugonjwa. Katika hatua hii hakuna dalili zozote za ugonjwa, lakini ukipima vipimo vya damu vinaonesha kuwa bado una maambukizi ya kaswende.
Hatua inayofuata ndiyo hatua ya mwisho ya ugonjwa. Ni hatua inayoonesha kuwa ugonjwa umekuwepo kwa miaka mingi sana. Kama umefikia hatu ya mwisho unaweza kuwa na vidonda vikubwa visivyopona. Vidonda hivi vikubwa vinaweza kuwa kwenye Ngozi au ndani ya mwili.
Unaweza pia kuwa na matatizo kwenye mishipa ya moyo na mishipa yad amu. Moja ya tatizo kubwa zaidi linaloweza kutokea ni ugonjwa wa kaswende kufika na kuharibu ubongo na mfumo wa fahamu. Ugonjwa huu unaweza kusababisha ukashindwa kusikia, kuona, kufikiri, na hata kifo.
Ugonjwa wa huu unatambuliwaje?
Kama una vidonda kwenye ngozi, daktari atakwangua gamba kutoka kwenye kidonda ili kuangalia chini ya darubini
Mara nyingi, madaktari wanategemea zaidi vipimo. Vpimo kadhaa vinaweza kuhitajika ili kuwa na uhakika kuwa una kaswende
Mji maji ya uti wa mgongo yanaweza kuchukuliwa kwa sindano ili kuyapima (spinal tap) kama kuna wasiwasi kuwa kaswende imefikia mfumo wa fahamu.
Kaswende inatibiwaje?
Ugonjwa wa kaswende unawea kutibiwa kwa sindano ya penicillin. Kama una mzio na penicillin, daktari anaweza kukupatia aina nyingine ya antibiotiki.
Jambo jingine la msingi la kukumbuka kama una kaswende?
Kwa sababu kaswende ni ugonjwa unaoenezwa kwa ngono, ni muhimu kuwa mwenzi wako akapimwe na kutibiwa pia. Ni vizuri pia kuongea na dakatari ili akupime na magonjwa mengine ya zinaa. Ongea na daktari ili utambue ni lini unaweza kuanza kushiriki ngono tena kwa usalama baada ya matibabu.
MAELEZO ZAIDI KUHUSU UGONJWA WA KASWENDE
Maelezo ya jumla
Ni ugonjwa unaosababisha kuwa na kidonda mwanzoni, baadae ugonjwa unasambaa kwenye ngozi na kwenye utando ute, kisha dalili zinakoma kwa muda mrefu, baadae sana kunatokea vidonda kwenye ngozi, mifupa, viungo vya mwili, mfumo wa fahamu na mfumo wa kusukuma damu.
Sababu ya ugonjwa wa kaswende
Treponema pallidum
Epidemiolojia ya ugonjwa wa kaswende
Unapatikana dunia nzima. Unawapata zaidi vijana wanaojihusisha na ngono wenye umri kati ya 20-29. Unapatikana zaidi katika maeneo ya mijini.
Uambukizo wa ugonjwa wa kaswende
Njia za kuambukizwa
- Mtu anaambukizwa akigusana moja kwa moja na vidonda hasa wakati wa ngono.
- Kugusa kwa bahati mabaya nyama au damu au kwa kuongezewa damu ya mtu mwenye maambukizi
- Kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto kabla hajazaliwa
Muda kabla dalili kuanza
Siku 10 mpaka miezi 3, kwa kawaida ni wiki 3
Muda wa uambukizo
Inategemea na haifahamiki mwisho lini, katika kipindi cha mwanzo na kipindi chote atakachopata vidonda kwenye ngozi au mdomo, vinavyokuja na kuondoka katika kipindi chote cha miaka 4 ya mwanzo. Katika kipindi hiki ambacho mgonjwa hapati dalili, hakuna uhakika ni kwa kiasi gani mtu anaweza kuambukiza wengine. Lakini kupatiwa matibabu na dawa ya penicillin kwa masaa 24-48 huondoa kabisa uwezo wa kuambukiza wengine.
Dalili za ugonjwa wa kaswende
Dalili za ugonjwa wa kaswende zimegawanyika katika hatua 3
- Dalili za awali
-
- Mgonjwa anapata kidonda kigumu kisicho na maumivu mahali ilipoingilia kaswende na pia kuvimba mtoki.
- Kidonda huwa ni kimoja, hakina maumivu na kinakuwa kwenye sehemu za siri au sehemu nyingine (midomo, ulimi, matiti) na kinapona chenyewe bila matibabu baada ya wiki 1
- Mtoki unavimba pande zote mbili na hakuna maumivu
- Dalili za hatua ya pili
-
- Baada ya wiki 4-6 ya dalili za awali, ugonjwa unasambaa mwili mzima.
- Anapata upele mwili mzima kwa muda mfupi na vipele haviwashi
- Vipele vinavyotokea mwanzo vinaweza kuambukiza ukivishika kwa sababu majimaji yake yanakuwa na vimelea wengi
- Dalili za hatua tatu
-
- Hatua hii inahusisha uharibifu mkubwa wa ngozi, mifupa, viungo vya mwili na sehemu zenye utando ute.
- Matatizo mengine yanatokea kwenye mfumo wa kusafirisha damu na mfumo wa fahamu
- Kaswende wakati wa ujauzito
-
- Kulingana na ukali wa kaswende ya mama, mtoto anaweza kuzaliwa na matatizo mengi, naweza kuzaliwa amekufa au mimba zikatoka mfululizo
Utambuzi wa ugonjwa wa kaswende
- Kipimo cha damu (serologic test)- hiki kinaweza kuonesha maambukizi wiki 6 -8 baada ya maambukizi
- Kupima sampuli ya kidonda cha ngozi inaweza kuonesha vimelea – Dark field microscopy
Matibabu ya ugonjwa wa kaswende
Matibabu yanategemea na hatua ya ugonjwa
- Matibabu ya hatua ya awali na pili
-
- Benzathin penicillin 2.4 M IU Im stat AU
- Tetracycline AU Erythromycin 500mg PO Qid for 2 weeks kwa watu wasiotumia penicillin
- Matibabu ya hatua ya tatu
-
- Benzathine benzylpenicillin (IM) 2.4MU once weekly for 3 consecutive weeks AND azithromycin (PO) 2g stat
- Kaswende wakati wa ujauzito
-
- Benzathine benzylpenicillin (IM) 2.4MU, as a single dose. In case of late syphilis 3 doses of benzathine benzylpenicillin should be provide
Kuzuia
- Toa matibabu kwa wagonjwa
- Tibu wapenzi wa wagonjwa pia
- Toa elimu kuhusu ngono salama
- Dhibiti magonjwa ya ngono kwa wanaouza milii (Malaya)
-
- Vipimo vya kila mwezi na kutoa matibabu
- Kuwagawia kondomu
- Kuchunguza wanawake wajawazito na kutoa matibabu mapema ili kuzuia kuambukiza mtoto
- Chunguza damu ya kuongeza watu kabla haijatumika
Leave feedback about this