Last Updated on October 12, 2023 by Dr Mniko
Je KIFUA KIKUU inaweza kutibiwa?
Karibu visa vyote vya KIFUA KIKUU siku hizi vinaweza kutibiwa na kupona. Ni muhimu kumeza dawa za KIFUA KIKUU kama ulivyoelekezwa kwa mpangilio na kwa kipindi chote cha matibabu. Watu wengi wenye KIFUA KIKUU huanza matibabu kwa kumeza walau aina nne za vidonge. Baada ya miezi kadhaa idadi ya vidonge inaweza kupunguzwa. Hivi vidonge vinaweza kutibu KIFUA KIKUU kama vikimezwa kwa angalau miezi 6.
Vidonge hutolewa kwa mgonjwa na chini ya uangalizi wa musimamizi, kwa kawaida anakuwa mtumishi wa huduma za afya mara 3 kwa wiki. Wakati mwingine, vijidudu vya KIFUA KIKUU vinakuwa sugu. Hii ina maana kwamba vidonge vya KIFUA KIKUU ambavyo mara nyingi hutumika kutibu KIFUA KIKUU vinashidwa kuua wadudu wa KIFUA KIKUU.
Hii ikitokea, mchanganyiko wa dawa zingine unatolewa. KIFUA KIKUU sugu ni vigumu kutibiwa na inachukua muda zaidi kudhibitiwa, lakini watu wengi wenye KIFUA KIKUU sugu wanaweza kutibiwa. Daktari atahakikisha vipimo maalum vinafanyika kwa kuangalia upinzani wa madawa.
Je dawa za KIFUA KIKUU ni salama?
Kama ilivyo kwa dawa zozote, Vidonge vya KIFUA KIKUU wakati mwingine husababisha madhara, hatahivyo watu wengi huwa hawapatwi na matatizo yoyote. Mwambie daktari wako au mfanyakazi wa huduma za afya mara moja kama ukiona ugonjwa wowote usiotarajiwa au kama dalili zifuatazo zikitokea:
- Kichefuchefu na / au kutapika
- Homa ya manjano (njano ngozi au macho, mkojo mweusi)
- Homa isiyoelezeka au kuchoka
- Ganzi au kufa ganzi ya mikono na miguu na maumivu ya pamoja
- Kuwashwa ngozi / ukurutu, upele
- Kiwaa au upofu wa kushindwa kuona rangi nyekundu / kijani
Ni muhimu kumweleza mtumishi wa afya kama unatumia dawa yoyote nyingine hasa ya uzazi wa mpango, vidonge vya kisukari, madawa ya kifafa, au vidonge vya kudhibiti msongo wa mawazo kwa sababu mwingiliano wa dawa unaweza kuleta madhara.
Rifampicin (moja ya madawa ya KIFUA KIKUU) husababisha kugeuka kwa mkojo, jasho na machozi kuwa rangi ya njano.
Kwa nini nalazimika kumeza vidonge kwa muda mrefu?
Unatakiwa kuhakikisha kwamba dawa zinaua wadudu wote wa KIFUA KIKUU. Baadhi ya wadudu wanaweza kuuawa wakati wa kuanza kutumia dawa lakini inachukua muda mrefu mpaka wadudu wote kufa.
Najisikia nafuu! Kwa nini niendelee kumeza vidonge vaya KIFUA KIKUU?
Hata baada ya kujisikia vizuri, usiache kumeza vidonge. Bado kuna wadudu wa KIFUA KIKUU katika mwili wako. Kama ukiacha kutumia vidonge vyako, wadudu ambao bado hawajafa wanaweza kuongezeka na unaweza kupata ugonjwa tena. KIFUA KIKUU sugu isiyotibika inaweza kujitokeza kama mtu hatumii dawa ya KIFUA KIKUU kama alivyoagizwa. Mtu aliye na ugonjwa wa KIFUA KIKUU sugu na hapati matibabu, anawea kusambaza aina hii ya vimelea sugu kwa watu wengine atakapokohoa au kupiga chafya.
Naweza kumeza dawa zangu namna gani?
Ni rahisi kukumbuka kumeza vidonge kama unavimeza wakati unaofanana kila siku. Pia ni bora kuvimeza kukiwa hakuna chochote tumboni, nusu saa kabla ya chakula au wakati wa kwenda kulala. Mtumishi wa Kituo atapanga namna ya kukupatia dozi ya dawa zako, kwa kawaida Jumatatu, Jumatano na Ijumaa.
Kama ukisahau kumeza vidonge mara nyingi dawa hazitafanya kazi. Utatakiwa kuendelea kumeza vidonge hadi umefidia dozi zote ulizokosa/ulizosahau kumeza. Unatakiwa pia:
- Kunywa vidonge kwa maji, maziwa, au glasi ya juisi.
- Mwambie daktari au mtumishi wa afya kuhusu dawa nyingine unazozitumia (ikiwa ni pamoja na vidonge vya kupanga uzazi).
- Epuka kulewa pombe wakati ukiwa unatibiwa KIFUA KIKUU. Pombe huongeza hatari ya matatizo makubwa ya ini kama ikitumiwa wakati ukiwa kwenye dawa za Kifua Kikuu.
- Kula chakula cha afya na lala muda wa kutosha.
Uchunguzi wa kila mwezi kwa mgonjwa wa KIFUA KIKUU
Wakati ukitumia dawa za Kifua Kikuu, ziara ya kila mwezi kwa daktari wa Kliniki ya KIFUA KIKUU inahitajika. Madhumuni ya ziara hii ni:
- Kuangalia uzito na afya kwa ujumla,
- Kuhakikisha mwili unaendelea kupona na kuangalia kama Xray yako ya kifua inaendelea kuboreka.
- Kuhakikisha huna madhara yoyote mabaya yatokanayo na dawa.
Naweza kuhakikisha namana gani kuwa KIFUA KIKUU haisambai?
- Dawa kwa kawaida itakuzuia kueneza vijidudu vya KIFUA KIKUU ndani ya wiki chache baada ya kuazna matibabu. Lakini kumbuka, wewe bado hujapona. Kitu muhimu zaidi ni kuendelea kutumia vidonge kama ulivyoagizwa hadi daktari akwambie kuwa unaweza kuacha
- Kila mara kumbuka kufunika mdomo unapokohoa na kupiga chafya.
- Waambie watu wote ambao hutumia muda mwingi pamoja na wewe kuwasiliana na Kliniki ya KIFUA KIKUU ili waweze kupimwa. Hii ni pamoja na ndugu wa familia, marafiki au wafanyakazi wenzako
Je naweza kuishi kama nilivyokuwa nikiishi?
Kama una KIFUA KIKUU inayoathiri mapafu au ugonjwa wa mkali, unaweza kutakiwa kulazwa hospitalini kwa wiki za mwanzo za matibabu ya KIFUA KIKUU. Mawasiliano na shughuli zako zitazuiliwa kwanza hadi daktari atakapokwambia kuwa hauumwi tena. Mara nyingi hali hii inadumu kwa wiki chache.
Wakati maambukizi yakiisha wagonjwa wengi wa KIFUA KIKUU huishi nyumbani na kuendelea na shughuli zao za kawaida. Wakati huwezi tena kuambukiza vijidudu vya KIFUA KIKUU, unaweza kukaribiana na mtu yeyote, ikiwa ni pamoja na watoto. Unaweza kuendelea na shughuli za mara kwa mara na kurudi kufanya kazi kama ukiwa unaendelea kutumia dawa
Leave feedback about this