Magonjwa ya ndani ya mwili

MAFUA YA NGURUWE:Sababu,dalili,matibabu

Mafua ya nguruwe (Swine flu) ni ugonjwa unaosababishwa na virusi aina ya H1N1 na H3N2 wanaosababisha mafua. Dalili za mafua ya nguruwe zinafanana kabisa na zile za mafua ya kawaida.
Mwaka 2009 wanasayansi walitambua aina ya kirusi kinachoitwa H1N1. Kirusi hiki kilikuwa kimetengenezwa kwa muunganiko wa virusi ambao wanapatikana kwa nguruwe, ndege na wanadamu na kusababisha ugonjwa kwa wanadamu. Kati ya mwaka 2009 -2010, virusi wa H1N1 walisababisha ugonjwa wa mafua kwa watu wengi. Kwa sababu watu wengi sana duniani kote waliugua mafua haya, shirika la afya duniani lilitangaza ugonjwa huu kuwa janga la dunia. Ilipofika agosti mwaka 2010 WHO ilitangaza kuwa janga limedhibitiwa.
Siku hizi kuna chanjo ambayo inaweza kulinda watu dhidi ya mafua ya nguruwe yanayosababishwa na H1N1.

Read More
X