Magonjwa ya ndani ya mwili

UGONJWA WA TAUNI:Sababu,dalili,matibabu,kuzuia

Last Updated on October 13, 2023 by Dr Mniko

Maelezo ya jumla

Ugonjwa wa tauni (plague) ni ugonjwa wa kuambukiza unaowapata  panya, wanyama wengine na binadamu. Ugonjwa huu husababishwa na bakteria wanaoitwa Yersinia pestis. Kuna aina tatu za ugonjwa huu, tauni inayosababisha mtoki (bubonic), tauni inayosababisha nyumonia (pneumonic) na tauni inayosambaa kwenye damu (septicemic). Dalili za ugonjwa huu ni pamoja na: homa, maumivu ya kichwa, kuhisi baridi, maumivu ya misuli, kichefuchefu na kutapika. Tauni inayosababisha mtoki husababisha tezi za limfu kuvimba; Tauni inayosababisha nyumonia husababisha matatizo kwenye mapafu; Tauni inayosambaa kwenye damu husababisha kuvuja damu na kuoza kwa tishu za mwili. Watu wanaoishi maeneo ya kijijini, wanaokutana na panya, wako katika hatari kubwa zaidi ya kuambukizwa ugonjwa huu. Ugonjwa huu hutambuliwa kwa ishara, dalili na vipimo vya maabara. Matatizo yanayoweza kutokea ni pamoja na; nyumonia, mshtuko na kifo. Wagonjwa 8-10% hufa hata baada ya matibabu kwa kutumia antibiotiki.

 Je, nini dalili za tauni?

Dalili za ugonjwa huu zinategemea mgonjwa ameambukizwaje bakteria wanaosababisha tauni.  Dalili huanza kuonekana siku 2 hadi 7, lakini zinaweza kuanza mapema zaidi kwa tauni inayosababisha nyumonia.
Kuna aina tatu za tauni:

  • ugonjwa unaosababisha mtoki (bubonic)- maambukizi ya tezi za limfu
  • Ugonjwa unaosababisha nyumonia (pneumonic) – maambukizi ya mapafu
  • Ugonjwa unaosambaa kwenye damu (septicemic) – Maambukizi kwenye damu

Tauni inayosababisha mtoki

Dalili huanza kuonekana ghafla, siku 2 – 5 baada ya kuambukizwa bakteria, na hujumuisha:

  • Homa ya ghafla
  • Uchovu
  • Maumivu ya kichwa
  • Kuhisi baridi
  • Kukosa nguvu
  • Maumivu ya misuli
  • Degedege
  • Kuuma na kuvimba kwa tezi za limfu (mtoki)
  • Tezi za limfu za kwenye kinena, makwapani shingoni huvimba na kusababisha mtoki kwenye kwapa, kinena au shingoni.
  • Maumivu yanaweza kutokea katika eneo lililoumwa kabla uvimbe haujaonekana

Tauni inayosababisha nyumonia

Dalili huanza ghafla siku 2 – 3 baada ya kuambukizwa, na hujumuisha:

Tauni inayosambaa kwenye damu

Aina hii inaweza kusababisha kifo hata kabla ya dalili zake kuonekana. Dalili hujumuisha:

Je, Tauni husababishwa na nini?

Ugonjwa huu husababishwa na bakteria wanaoitwa yersinia pestis. Mnyama mgugunaji, kama panya, anapokuwa na vimelea wa ugonjwa huu, viroboto wake wanaeneza ugonjwa huu wanaporuka na kuwauma wanyama wengine
Wanadamu huambukiwa tauni kwa njia zifuatazo:

  • Kuumwa na viroboto
    • Mara nyingi watu huambukizwa ugonjwa huu baada ya kuumwa na kiroboto aliyeambukizwa.
    • Wakati wa mlipuko wa ugonjwa huu, wanyama wagugunaji kama panya hufa kwa wingi, na viroboto wao hutoka na kutafuta vyanzo vingine vya damu.
    • Watu na wanyama wanaotembelea maeneo ambapo panya wamekufa kwa tauni huwa katika hatari ya kuumwa na viroboto wa panya hao na kuambukizwa.
    • Mbwa na paka pia wanaweza kubeba viroboto walioambukizwa na kuwaleta nyumbani.
    • Baada ya kuumwa na kiroboto unaweza kupata tauni inayosababisha mtoki au inayosambaa kwenye damu.
  • Kugusa majimaji au tishu zenye maambukizi
    • Wanadamu wanaweza kuambukizwa baada ya kugusa tishu au majimaji ya mwili wa mnyama aliyeambukizwa ugonjwa huu.
    • Matone yenye uambukizo
  • Mtu mwenye tauni inayosababisha nyumonia, akikohoa anarusha matone ya mate kwenye hewa yenye maambukizi. Mtu mwingine akivuta hewa yenye matone haya anaweza kuambukizwa tauni inayosababisha nyumonia.
    • Mtu aliyekaribu na mgonjwa wa tauni inayosababisha nyumonia ni rahisi kuambukizwa.
    • Matone kwenye hewa baada ya kukohoa au kupiga chafya ndio njia pekee ya mwanadamu kumwambukiza mwingine tauni.
    • Paka yuko katika hatari kubwa zaidi ya kuambukizwa ugonjwa huu kwa sbabu anaweza kula mizoga ya panya na kuambukizwa tauni kisha kuwaambukiza wanadamu.

Nani yuko katika hatari zaidi?

Tauni hutokea kwenye maeneo yenye wanyama wagugunaji kama panya. Hatari ni kubwa zaidi kwa watu wanaoishi vijijini, hasa wanaoishi katika maeneo yenye vicheche, panya n.k.
Watu wanaweza kupata ugonjwa huu kwa kuumwa na viroboto wa wanyama wagugunaji wanaobeba bakteria wanaosababisha tauni. Watu walio katika hatari kubwa ya kuambukizwa ni pamoja na:

  • Watu wanaoshughulika na wanyama walioambukizwa
  • Watu huwa katika hatari zaidi, muda mfupi baada ya mlipuko wa taun.
  • Watu wanaotembelea maeneo yenye panya waliokufa kutokana na ugonjwa huu.
  • Watu wenye paka walioambukizwa taun

Wakati gani utafute Matibabu ya haraka?

Watu wanaopaswa kutafuta huduma ya matibabu haraka ni pamoja na:

  • Mtu yeyote ambaye ameanza kuona dalili za tauni baada ya kuumwa na viroboto, hasa baada ya kutembelea eneo lenye mlipuko.

Watu walio karibu au wanaoishi na wagonjwa wa tauni ya mapafu, wanapaswa kuchunguzwa , na ikiwezekana kuwekwa chini ya unagalizi. Dawa za antibiotiki zinaweza kutolewa pia kama kinga.

tauni

Utambuzi

Hatua ya kwanza ya kutambua ugonjwa huu ni kuchunguzwa na daktari. Ishara ya tauni inayosababisha mtoki ni kuvimba na maumivu ya tezi za limfu. Kuwepo kwa mtoki na historia ya kuumwa na viroboto humsaidia daktari kufanya utambuzi.
Mara nyingi mgonjwa wa tauni inayosambaa kwenye damu na inayosababisha nyumonia hana dalili zilizo wazi ambazo huonesha kuwa ana ugonjwa. Utambuzi hufanyika kwa kuchukua sampuli kutoka kwa mgonjwa, hasa damu au sehemu ya tezi ya limfu iliyovimba, na kuipima maabara.
Mara baada ya maabara kupokea sampuli, matokeo ya awali ya vipimo yanaweza kuwa tayari ndani ya masaa mawili. Ili kudhibitisha matokeo haya inaweza kuchukua masaa 24 hadi 48.
Mara nyingi, kama mgonjwa anahisiwa kuwa na tauni,  matibabu ya awali kwa kutumia antibiotiki huanzishwa kabla matokeo ya vipimo.

Uchaguzi wa matibabu

Huu ni ugonjwa mbaya sana, lakini hutibiwa vyema kwa antibiotiki za kawaida. Mgonjwa anapaswa kutibiwa mapema ili kupunguza uwezekano wa kupata matatizo yanayotokana na taunii.
Watu walio karibu na wagonjwa wa tauni inayosababisha nyumonia wanaweza kufanyiwa tathmini na hata kuwekwa chini ya uangalizi. Wanaweza pia kupewa antibiotiki ili kuzuia kutokea kwa dalili kama wameambukizwa.
Wagonjwa wanapaswa kupewa matibabu mapema sana. Kama mgonjwa hatapata matibabu ndani ya masaa 24 baada ya dalili za awali kuanza, anaweza kufa. Dawa za antibiotiki zinazoweza kutibu ugonjwa huu ni pamoja na:

  • Streptomycin
  • Gentamicin
  • Doxycycline
  • Ciprofloxacin

Mgonjwa anaweza kuhitaji kuongezewa maji, oksijeni, au hata msaada kupumua.
Wagonjwa wenye tauni inayosababisha nyumonia wanapaswa kutengwa na wagonjwa wengine. Wahudumu wa afya wanapaswa kujikinga vyema ili wasiambukizwe. Watu waliokuwa karibu na wagonjwa wenye ugonjwa wa mapafu wanapaswa kuwekwa chini ya uangalizi na kupewa antibiotiki ili kudhibiti maambukizi mapema.

Nini cha kutarajia?

Bila matibabu, 50% ya watu walio na ugonjwa unaosababisha mtoki hufa. Karibu watu wote wenye ugonjwa unaosababisha nyumonia hufa kama hawatatibiwa. Matibabu hupunguza vifo kwa 8-10%.

Matatizo yanayoweza kutokea

Matatizo yanayoweza kutokea ni pamoja na:

  • Nyumonia
  • Kuenea kwa maambukizi mwili mzima
  • Kifo kama hutatibiwa

Kuzuia

Hatua muhimu za kuzuia maambukizi ni pamoja na:

  • Kupunguza panya wanaoishi karibu na nyumba, sehemu kazi au maeneo ya michezo. Ondoa vichaka, miamba, uchafu, kuni zilizotapakaa, na chochote kinachoweza kuwa chakula cha panya.
  • Vaa glavu kama unamshughulikia mnyama mwenye viroboto ili kupunguza uwezekano wa kuambukizwa tauni.
  • Jipake dawa ya kufukuza viroboto (repellant) kama unaenda katika maeneo hatarishi, mfano kuweka kambi mwituni, kupanda mlima au kufanya kazi msituni.
  • Hakikisha hakuna viroboto kwa wanyama wako wa kufugwaa. Wasafishe kwa dawa mara kwa mara. Usiwaache wanyama wako kuzururazurura wanaweza kubeba viroboto na kuwaleta nyumbani.
  • Kama mnyama wako wa kufugwa akiugua mpeleke kwa daktari wa mifugo mapema iwezekanavyo.

MAELEZO ZAIDI KUHUSU UGONJWA WA TAUNI

Maelezo ya jumla

Ni maambukizi mabaya ya bakteria yanayoweza kusambaa na kuua watu wengi sana kwa muda mfupi

Sababu ya ugonjwa wa tauni

Yersinia pestis

Epidemiolojia

Tauni inapatikana kwa panya buku wanaishi kwenye misitu minene. Tauni ya msituni inapatikana mashariki mwa Marekani, maeneo mengi ya Amerika kusini, Kasikazini, kati, mashariki na kusini mwa Afrika, kati na kusini mashariki mwa bara Asia. Lakini ugonjwa tauni unaowaathiri watu, umedhibitiwa kwa sehemu nyingi za dunia

Panya buku wa msituni wanabeba vimelea wa tauni. Wanyama wanaokula nyama na paka wa kufugwa wanaweza kuwa chanzo cha maambukizi kwa watu.

Uambukizo wa ugonjwa wa tauni

Kwa kung’atwa na kupe mwenye maambukizi. Kwa kushika tishu za mnyama aliyeambukizwa.

Muda kabla dalili kuanza

Siku 1-7

Muda wa uambukizo wa tauni

Kupe wanaweza kuendelea kuambukiza watu kwa miezi kadhaa kama mazingira sahihi ya joto na unyevunyevu.  Tauni inayosababisha majiu sio rahisi kusambaa isipokuwa kama mtu ameshika majipu yaliyopasuka. Tauni inayoshambulia mapafu inaweza kusambaa kwa urahisi kwa mazingira na hali ya hewa vinaruhusu. Msongamano unachangia maambukizi kuenea.

Nani yuko kwenye hatari

Watu wote wako kwenye hatari. kinga baada ya kuugua na kupona ni ya muda na inaweza isikukinge na maambukizi

Dalili za ugonjwa wa tauni

  1. Tauni inayosababisha mtoki/majipu – inasababisha kuvimba kwa tezi za limfu (bubos); zaidi tezi za kwenye kinena, wakati mwingine za kwenye makwapa au sehemu nyingine. Uvimbe unaweza kuwa ukubwa way ai, unaouma au unaweza usiume. Dalili nyingine ni pamoja na:
  1. Tauni unaathiri mapafu
    • Dalili zinaanza ghafla
    • Uchovu
    • Kutoa makohozi ya maji maji baadae makohozi yenye damu
    • Kujaa kwa maji kwenye mapafu
    • Kifo baada ya siku 1-2

Utambuzi wa ugonjwa wa tauni

  • kwa kuchunguza makohozi au usaha – gram negative bacilli

Matibabu ya ugonjwa wa tauni

  1. Matibabu ya haraka kwa kutumia antibiotiki kama streptomycin au tetracycline

Kuzuia ugonjwa wa tauni

  1. Matibabu ya wagonjwa
  2. Kutoa tiba kinga kwa watu wote waliokuwa karibu na mgonjwa kwa kutumia –sulfa
  3. Eneo ambapo ugonjwa umetokea linapaswa kuwekwa karantini
  4. Puliza dawa za kuua kupe
  5. Wahimize watu kuua paka
  6. Toa taarifa kwa mamlaka zinazohusika

Vyanzo

https://medlineplus.gov/ency/article/000596.htm

Leave feedback about this

  • Quality
  • Price
  • Service

PROS

+
Add Field

CONS

+
Add Field
Choose Image
Choose Video
X