Maelezo ya jumla
Ugonjwa wa homa ya ini A ni ugonjwa wa ini unaosababishwa na virusi wanaoitwa hepatitis A.
Dalili za ugonjwa wa homa ya ini A
Homa huanza ghafla, uchovu, kupoteza hamu ya chakula na kichefuchefu. Mkojo unaweza kuwa na rangi kama chai au soda ya cocacola, kinyesi chenye rangi iliyofifia, na manano kwenye macho au ngozi hutokea siku chache baadae. Watoto wengi wenye umri chini ya mika 6 haoneshi dalili zozote baada ya kuambukizwa. Mara nyingi watoto wakubwa na watu wazima wanapoambukizwa, hupata dalili, hii ni pamoja na manjano.
Jinsi ugonjwa unavyoambukizwa
Virusi wa hepatitis A wanasambazwa na kinyesi. Kama ukishika kinyesi au kitu kilichochafuliwa na kinyesi na kisha ukashika au kuweka vidole au kitu kilichochafuliwa mdomoni utaambukizwa virusi vya hepatitis A. Mammbukizi haya yanaweza kusambaa kama watu hawanawi mikono baada ya kutoka chooni na kisha kushika au kuandaa chakula.
Kumbuka kuwa mtu aliyeambukizwa asiyekuwa na dalili yoyote anaweza bado kukuambukiza ugonjwa huu.
Inachukua muda gani dalili kuanza kuonekana
Inaweza kuchukua siku 15 mpaka 50, kwa kawaida siku 28, toka ulipoambukizwa mpaka unapoanza kuona dalili.
Wakati gani unaweza kuambukiza wengine ugonjwa wa homa ya ini A
Unaweza kuambukiza wengine ugonjwa huu kuanzia wiki ya 2 kabla ya dalili kuanza mpaka wiki mbili baada ya dalili kuanza. Hatari ya kuambukiza wengine inapungua sana baada ya manjano kuanza.
Utambuzi wa ugonjwa wa homa ya ini A
Utafanyiwa kipimo cha damu (Hepatitis A IgM antibody test) ili kuangalia kama umepatwa na maambukizi hivu karibuni.
Matibabu ugonjwa wa homa ya in A
Hakuna matibabu maalum ya kutibu ugonjwa huu.
Kujikinga au kuzuia ugonjwa wa homa ya ini A
Chanjo ya hepatitis A inapendekezwa kwa watoto wa miezi 12 mpaka 23 na inashauriwa kwa watu walio kwenye hatari zaidi ya kuambukizwa. Watu wanaosafiri kwenda maeneo yenye maambukizi kwa wingi, wanaume wanaoshiriki ngono na wanaume wenzao, watumiaji wa madawa ya kulevya na watu wanaofanya kazi zinazowaweka kwenye hatari ya kuambukizwa. Chanjo inashauriwa pia kwa watu wenye ugonjwa wa ini kwa sababu wako kwenye hatari ya kupata ugonjwa mkali zaidi.
- Nawa mikono vizuri baada ya kutoka chooni na kabla ya kula au kuandaa chakula
- Safisha kwa uangalifu vyoo na maeneo yanayozunguka vyoo kwa angalau mara 1 kwa siku
Angalia pia:
- Ugonjwa wa homa ya ini B: https://wikielimu.com/ugonjwa-wa-homa-ya-ini-b/
- Ugonjwa wa homa ya ini C: https://wikielimu.com/ugonjwa-wa-homa-ya-ini-c/
MAELEZO ZAIDI KUHUSU HOMA YA INI A
Maelezo ya jumla
Ni ugonjwa unaosababishwa na virusi unaosababisha homa ya ghafla, uchovu, kichefuchefu na maumivu ya tumbo yanayofuatiwa na manjano kwenye macho au midomo baada ya siku chache.
Sababu
Virusi vya Hepatitis A
Epidemiolojia
Ni ugonjwa unaopatikana duniani kote, na kwa baadhi ya maeneo unatokea kama ugonjwa wa mlipuko. Kwa mataifa yaliyoendelea, watu wazima kwa kawaida wanakuwa wamejenga kinga dhidi ya homa ya ini A na milipuko inakuwa si kawaida. Maambukizi yanatokea zaidi katika maeneo yenye usafi duni na unatokea zaidi katika umri mdogo.
Njia ya uambukizo
- Kutoka kwa mtu mmoja mpaka mwingine kwa kushika mikono ya mtu ambaye hakunawa vizuri
- Kupitia chakula au maji yaliyochafuliwa na watu wanaoviandaa.
Muda kabla ya dalili kuanza kuonekana
Siku 15-55. kwa wastani ni siki 28-30
Muda wa uambukizo
Uwezo wa kuambukiza wengine ni mkubwa zaidi siku 15 kabla ya dalili kuanza kuonekana na kuendelea kwa siku kadhaa baada ya manjano kuanza. Kwa watu wengi, hawawezi kuambukiza wengine wiki moja baada ya kupata manjano.
Nani yuko kwenye hatari zaidi
Watu wote wako kwenye hatari ya kuambukizwa. Kinga baada ya kuambukizwa inaweza kuendelea kuwepo maisha yote.
Dalili
- Homa ya ghafla, uchovu, kichefuchefu na maumivu ya tumbo, na baadae manjano baada ya siku kadhaa.
- Mgonjwa hupona kabisa bila shida yoyote
Utambuzi
- Kwa kuangalia dalili na ishara
- Kwa kupima kuangalia uwepo wa IgM (IgM anti-HAV) kwenye damu ya watu wenye ugonjwa au waliugua hivi karibuni
Matibabu
Kutibu dalili: mapumziko, kula mlo wenye wanga kwa wingi, mafuta kidogo na protini
Kuzuia
- Elimu kwa uma kuhusu usafi wa mazingira na usafi binafsi, kwa kukazia unawaji wa mikono na matumizi ya choo.
- Uwepo wa maji safi na salama na yakingwe yasiingiliwe na kinyesi
- Watu wanaosafiri kwenda kwenye maeneo yenye mlipuko wapwe chanjo
Leave feedback about this